Mhubiri 11 - Swahili Common Language DC Bible

Afanyavyo mwenye busara

1Jishughulishe na biashara

hata kama kwa kubahatisha;

yawezekana baadaye

ukapata chochote kile.

2Wagawie watu saba hata wanane sehemu yako,

maana, hujui balaa litakalofika duniani.

3Mawingu yakijaa maji, mvua hunyesha;

mti ukiangukia kusini au kaskazini,

hapo uangukiapo ndipo ulalapo.

4Anayengoja upepo hatapanda mbegu,

anayesubiri mawingu yatoweke, hatavuna kitu.

5Usivyojua jinsi uhai unavyoingia katika mifupa ya mtoto tumboni mwa mamake, kadhalika huwezi kuelewa matendo ya Mungu, ambayo hufanya kila kitu.

6Panda mbegu asubuhi na jioni usiache kupanda, maana, hujui zipi zitaota; za asubuhi, za jioni, au zote zitakuwa nzuri.

7Mwanga wafaa, na kuliona jua kwapendeza macho.

8Mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kuwa siku za giza zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.

Mawaidha kwa vijana

9Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako, uchangamke wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na upeo wa macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.

10Ondoa mahangaiko moyoni mwako, jikinge, usipate maumivu mwilini kwa sababu ujana na mwisho wa maisha ni bure kabisa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help