Zaburi 129 - Swahili Common Language DC Bible

Sala dhidi ya maadui wa Israeli(Wimbo wa Kwenda Juu)

1“Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu

Kila mtu katika Israeli na aseme:

2“Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu,

lakini hawakufaulu kunishinda.

3Walinijeruhi vibaya mgongoni mwangu,

wakafanya kama mkulima anayelima shamba.

4Lakini Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu;

amezikata kamba za hao watu waovu.”

5Na waaibishwe na kurudishwa nyuma,

wote wale wanaouchukia mji wa Siyoni.

6Wawe kama nyasi juu ya paa la nyumba,

ambazo hunyauka kabla hazijakua,

7hakuna anayejishughulisha kuzikusanya,

wala kuzichukua kama matita.

8Hakuna apitaye karibu atakayewaambia:

“Mwenyezi-Mungu awabariki!

Twawabariki kwa jina la Mwenyezi-Mungu!”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help