Isaya 65 - Swahili Common Language DC Bible

Mungu huwaadhibu waasi

1 litakuwa mapumziko ya mifugo

kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.

11“Lakini nitafanya nini na nyinyi

mnaoniacha mimi Mwenyezi-Mungu,

msioujali Siyoni, mlima wangu mtakatifu,

nyinyi mnaoabudu mungu ‘Gadi’,

na kumtolea tambiko ya divai mungu ‘Meni’?

12Nimewapangia kifo kwa upanga,

nyote mtaangukia machinjoni!

Maana, nilipowaita, hamkuniitikia;

niliponena, hamkunisikiliza.

Mlitenda yaliyo maovu mbele yangu,

mkachagua yale nisiyoyapenda.

13Basi, mimi Mwenyezi-Mungu nasema,

watumishi wangu watakula,

lakini nyinyi mtaona njaa;

watumishi wangu watakunywa,

lakini nyinyi mtaona kiu;

watumishi wangu watafurahi,

lakini nyinyi mtafedheheka.

14Watumishi wangu wataimba kwa furaha moyoni,

lakini nyinyi mtalia kwa uchungu moyoni

na kupiga kelele kwa uchungu mkubwa rohoni.

15Wale niliowachagua nitawapa jina jipya.

Lakini nyinyi jina lenu watalitumia kulaania;

‘Watasema: Bwana Mungu awaue kama hao.’

16Basi, mwenye kujitakia baraka nchini,

atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli.

Mwenye kuapa katika nchi hii,

ataapa kwa Mungu wa kweli.

Maana taabu za zamani zimepita

zimetoweka kabisa mbele yangu.

Ulimwengu mpya

17 Taz Isa 66:22; 2 Pet 3:13; Ufu 21:1 “Sasa, naumba mbingu mpya na dunia mpya.

mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.

18Furahini, mkashangilie milele,

kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba.

Yerusalemu nitaufanya mji wa shangwe,

na watu wake watu wenye furaha.

19 Taz Ufu 21:4 Nami nitaufurahia mji wa Yerusalemu,

nitawafurahia watu wangu.

Sauti ya kilio haitasikika tena,

kilio cha taabu hakitakuwako.

20Hakutakuwa tena na vifo vya watoto wachanga,

wazee nao hawatakufa kabla ya wakati wao.

Akifa mtu wa miaka 100 amekufa akiwa kijana;

na akifa kabla ya miaka 100 ni balaa.

21Watu watajenga nyumba na kuishi humo;

watalima mizabibu na kula matunda yake.

22Hawatajenga nyumba zikaliwe na watu wengine,

wala kulima chakula kiliwe na watu wengine.

Maana watu wangu niliowachagua

wataishi maisha marefu kama miti;

wateule wangu watafurahia matunda ya jasho lao.

23Kazi zao hazitakuwa bure,

wala hawatazaa watoto wa kupata maafa;

maana watakuwa waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu,

wamebarikiwa wao pamoja na wazawa wao.

24Hata kabla hawajaniita, mimi nitawaitikia;

kabla hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.

25 Taz Isa 11:6-9 Mbwamwitu na kondoo watakula pamoja,

simba watakula nyasi kama ng'ombe,

nao nyoka chakula chao kitakuwa vumbi.

Katika mlima wangu wote mtakatifu,

hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu.

Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help