Zaburi 3 - Swahili Common Language DC Bible

Kuomba msaada asubuhi(Zaburi ya Daudi alipomkimbia Absalomu)

1Ee Mwenyezi-Mungu, tazama walivyo wengi adui zangu,

ni wengi mno hao wanaonishambulia.

2Wengi wanasema juu yangu,

“Hatapata msaada kwa Mungu.”

3Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu u ngao yangu kila upande;

kwako napata fahari na ushindi wangu.

4Nakulilia kwa sauti, ee Mungu,

nawe wanisikiliza kutoka mlima wako mtakatifu.

5Nalala na kupata usingizi,

naamka tena maana wewe ee Mwenyezi-Mungu wanitegemeza.

6Sitayaogopa maelfu ya watu,

wanaonizingira kila upande.

7Uje ee Mwenyezi-Mungu!

Niokoe ee Mungu wangu!

Wewe wawavunja mataya maadui zangu wote;

wawavunja meno waovu wasinidhuru.

8Mwenyezi-Mungu ndiwe uokoaye;

uwape baraka watu wako.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help