1“Wakati huo na siku hizo
nitakapoirekebisha hali ya Yuda na Yerusalemu,
2nitayakusanya mataifa yote,
niyapeleke katika bonde liitwalo,
‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu.
Huko nitayahukumu mataifa hayo,
kwa mambo yaliyowatendea watu wangu Israeli,
hao walio mali yangu mimi mwenyewe.
Maana waliwatawanya miongoni mwa mataifa,
waligawa nchi yangu
3na kugawana watu wangu kwa kura.
Waliwauza wavulana ili kulipia malaya,
na wasichana ili kulipia divai.
4
19“Misri itakuwa mahame,
Edomu itakuwa jangwa tupu,
kwa sababu waliwashambulia watu wa Yuda
wakawaua watu wasio na hatia.
20Bali Yuda itakaliwa milele,
na Yerusalemu kizazi hata kizazi.
21Nitawaadhibu waliomwaga damu ya watu wa Yuda
wala sitawaachia wenye hatia.
Mimi, Mwenyezi-Mungu nakaa Siyoni.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.