Zaburi 6 - Swahili Common Language DC Bible

Sala wakati wa taabu(Kwa Mwimbishaji: Na ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi)

1 Taz Zab 38:1 Ee Mwenyezi-Mungu, usinikemee kwa hasira yako;

usiniadhibu kwa ghadhabu yako.

2Unihurumie, ee Mwenyezi-Mungu, nimeishiwa nguvu;

uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nataabika mpaka mifupani.

3Ninahangaika sana rohoni mwangu.

Ee Mwenyezi-Mungu, utakawia mpaka lini?

4Unigeukie, ee Mwenyezi-Mungu, uniokoe;

unisalimishe kwa sababu ya fadhili zako.

5Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka;

huko kuzimu ni nani awezaye kukusifu?

6Niko hoi kwa kilio cha uchungu;

kila usiku nalowesha kitanda changu kwa machozi;

kwa kulia kwangu naulowesha mto wangu.

7Macho yangu yamechoka kwa huzuni;

yamefifia kwa kutaabishwa na adui.

8 Taz Mat 7:23; Luka 13:27 Ondokeni kwangu enyi nyote watenda maovu!

Maana Mwenyezi-Mungu amesikia kilio changu.

9Mwenyezi-Mungu amesikia ombi langu;

Mwenyezi-Mungu amekubali sala yangu.

10Maadui zangu wote wataaibika na kufadhaika;

watarudi nyuma na kuaibishwa ghafla.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help