1 Timotheo UTANGULIZI - Swahili, Common Language Bible

UTANGULIZITimotheo alikuwa mwana wa mama mmoja Myahudi na baba yake alikuwa Mgiriki. Katika kitabu cha Matendo ya Mitume na katika barua nyingine za Paulo, tunajua kwamba Timotheo aliandamana na Paulo katika ziara zake na kumsaidia katika kazi yake ya kuhubiri Habari Njema (taz Mate 17:14-15; 18:5; 19:22 na 1Kor 4:17; 16:10-11; Fil 2:19-24; n.k.). Barua hii ya kwanza na ile ya pili pamoja na barua kwa Tito zaitwa pia barua za “kichungaji” kwa vile zinawapa mwongozo hao “wachungaji” au viongozi wa Kanisa.Barua hii ya kwanza kwa Timotheo yahusu mambo matatu makubwa:Kwanza Paulo anaonya jumuiya ya Wakristo ijihadhari na mafundisho ya uongo yaliyochanganya fikira za Kiyahudi na za watu wasio Wayahudi, mafundisho ambayo yalikuwa yanaendelezwa na baadhi ya watu. Baadhi ya mafundisho hayo yaliwaaminisha watu kwamba ulimwengu huu unaoonekana ni mbaya na kwamba mtu anaweza tu kuokoka kwa kujua siri fulani ambazo wamepewa tu watu fulani. Zaidi ya hayo watu walitakiwa kufuata mazoezi yaliyohusika na kuacha kula vyakula fulanifulani. Kisha Paulo anatoa mwongozo kuhusu ibada, muundo na mpango katika jumuiya ya Wakristo au Kanisa na tabia ya viongozi wake.Mwisho anatoa mashauri yake kwa Timotheo kuhusu namna ya kutekeleza utumishi wake na kujishughulisha na makundi mbalimbali ya waumini ili apate kuwa kweli “mtumishi mwema wa Kristo Yesu” (4:6).
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help