Isaya 5 - Swahili, Common Language Bible

Wimbo wa shamba la mizabibu

1 nane tu za divai;

anayepanda kilo 100 za mbegu

atavuna kilo 10 tu za nafaka.”

11Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema

wapate kukimbilia kunywa kileo;

wanaokesha hata usiku,

mpaka divai iwaleweshe!

12Katika karamu zao, hapakosekani vinubi,

zeze, matari, filimbi na divai.

Lakini hawajali matendo ya Mwenyezi-Mungu,

wala kuzitambua kazi za mikono yake.

13Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa uhamishoni

kwa sababu ya utovu wao wa akili.

Watu wenu mashuhuri watakufa njaa,

watu wengi watakufa kwa kiu.

14Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa,

imepanua kinywa chake mpaka mwisho.

Waheshimiwa pamoja na raia wa Yerusalemu

wanaingia humo makundi kwa makundi,

kadhalika na wote wanaousherehekea.

15Kila mtu atafedheheshwa,

na wenye kiburi wote wataaibishwa.

16Lakini Mwenyezi-Mungu wa majeshi atatukuzwa.

Yeye huonesha ukuu wake

kwa matendo yake ya haki,

kwa kuwahukumu watu wake.

17Wanakondoo, wanambuzi na ndama,

watapata malisho yao kwenye magofu ya miji yao,

kana kwamba hizo ni sehemu za malisho yao.

18Ole wao wanaoburuta uovu kama kwa kamba;

wanaokokota dhambi kama kwa kamba za mkokoteni.

19Wanasema:

“Mwache Mwenyezi-Mungu afanye haraka,

tunataka kuyaona aliyosema atayafanya!

Mtakatifu wa Israeli na atimize kusudi lake.

Hebu na tuone ana mipango gani!”

20Ole wao wanaosema uovu ni wema

na wema ni uovu.

Giza wanasema ni mwanga

na mwanga wanasema ni giza.

Kichungu wanasema ni kitamu

na kitamu wanakiona kuwa kichungu.

21Ole wao wanaojiona kuwa wenye hekima

ambao wanajiona kuwa wenye akili.

22Ole wao mabingwa wa kunywa divai,

hodari sana wa kuchanganya vileo.

23Kwa hongo kidogo wanawaachilia wenye hatia

na kuwanyima wasio na hatia haki yao.

24Kwa hiyo, kama moto uteketezavyo nyasi,

kama majani yateketeavyo katika mwali wa moto

ndivyo na mizizi yao itakavyooza,

na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama vumbi.

Maana wameiacha sheria ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi,

wamedharau neno la yule Mtakatifu wa Israeli.

25Kwa hiyo hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwawakia watu wake,

akaunyosha mkono wake dhidi yao, akawachapa,

hata milima ikatetemeka,

maiti zao zikawa kama takataka

katika barabara za mji.

Hata hivyo, hasira yake haikutulia,

mkono wake bado ameunyosha kuwaadhibu.

26Mwenyezi-Mungu analiashiria taifa la mbali;

anawapigia mruzi watu kutoka miisho ya dunia;

nao waja mbio na kuwasili haraka!

27Hawachoki wala hawajikwai;

hawasinzii wala hawalali;

hakuna mshipi wao uliolegea

wala kamba ya kiatu iliyokatika.

28Mishale yao ni mikali sana,

pinde zao zimevutwa tayari.

Kwato za farasi wao ni ngumu kama mawe;

mwendo wa magurudumu ya magari ni kimbunga.

29Askari wao wananguruma kama simba;

wananguruma kama wanasimba

ambao wamekamata mawindo yao

na kuwapeleka mahali mbali

ambapo hakuna awezaye kuwanyanganya.

30Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli

kama mvumo wa bahari iliyochafuka.

Atakayeiangalia nchi kavu

ataona giza tupu na dhiki,

mwanga utafunikwa na mawingu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help