1 nane tu za divai;
anayepanda kilo 100 za mbegu
atavuna kilo 10 tu za nafaka.”
11Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema
wapate kukimbilia kunywa kileo;
wanaokesha hata usiku,
mpaka divai iwaleweshe!
12Katika karamu zao, hapakosekani vinubi,
zeze, matari, filimbi na divai.
Lakini hawajali matendo ya Mwenyezi-Mungu,
wala kuzitambua kazi za mikono yake.
13Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa uhamishoni
kwa sababu ya utovu wao wa akili.
Watu wenu mashuhuri watakufa njaa,
watu wengi watakufa kwa kiu.
14Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa,
imepanua kinywa chake mpaka mwisho.
Waheshimiwa pamoja na raia wa Yerusalemu
wanaingia humo makundi kwa makundi,
kadhalika na wote wanaousherehekea.
15Kila mtu atafedheheshwa,
na wenye kiburi wote wataaibishwa.
16Lakini Mwenyezi-Mungu wa majeshi atatukuzwa.
Yeye huonesha ukuu wake
kwa matendo yake ya haki,
kwa kuwahukumu watu wake.
17Wanakondoo, wanambuzi na ndama,
watapata malisho yao kwenye magofu ya miji yao,
kana kwamba hizo ni sehemu za malisho yao.
18Ole wao wanaoburuta uovu kama kwa kamba;
wanaokokota dhambi kama kwa kamba za mkokoteni.
19Wanasema:
“Mwache Mwenyezi-Mungu afanye haraka,
tunataka kuyaona aliyosema atayafanya!
Mtakatifu wa Israeli na atimize kusudi lake.
Hebu na tuone ana mipango gani!”
20Ole wao wanaosema uovu ni wema
na wema ni uovu.
Giza wanasema ni mwanga
na mwanga wanasema ni giza.
Kichungu wanasema ni kitamu
na kitamu wanakiona kuwa kichungu.
21Ole wao wanaojiona kuwa wenye hekima
ambao wanajiona kuwa wenye akili.
22Ole wao mabingwa wa kunywa divai,
hodari sana wa kuchanganya vileo.
23Kwa hongo kidogo wanawaachilia wenye hatia
na kuwanyima wasio na hatia haki yao.
24Kwa hiyo, kama moto uteketezavyo nyasi,
kama majani yateketeavyo katika mwali wa moto
ndivyo na mizizi yao itakavyooza,
na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama vumbi.
Maana wameiacha sheria ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
wamedharau neno la yule Mtakatifu wa Israeli.
25Kwa hiyo hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwawakia watu wake,
akaunyosha mkono wake dhidi yao, akawachapa,
hata milima ikatetemeka,
maiti zao zikawa kama takataka
katika barabara za mji.
Hata hivyo, hasira yake haikutulia,
mkono wake bado ameunyosha kuwaadhibu.
26Mwenyezi-Mungu analiashiria taifa la mbali;
anawapigia mruzi watu kutoka miisho ya dunia;
nao waja mbio na kuwasili haraka!
27Hawachoki wala hawajikwai;
hawasinzii wala hawalali;
hakuna mshipi wao uliolegea
wala kamba ya kiatu iliyokatika.
28Mishale yao ni mikali sana,
pinde zao zimevutwa tayari.
Kwato za farasi wao ni ngumu kama mawe;
mwendo wa magurudumu ya magari ni kimbunga.
29Askari wao wananguruma kama simba;
wananguruma kama wanasimba
ambao wamekamata mawindo yao
na kuwapeleka mahali mbali
ambapo hakuna awezaye kuwanyanganya.
30Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli
kama mvumo wa bahari iliyochafuka.
Atakayeiangalia nchi kavu
ataona giza tupu na dhiki,
mwanga utafunikwa na mawingu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.