1Sikieni mafundisho yangu, enyi watu wangu;
yategeeni sikio maneno ya kinywa changu.
2
49Aliacha hasira yake kali iwawakie,
ghadhabu, chuki na dhiki,
na kundi la malaika waangamizi.
50Aliachilia hasira yake iendelee,
wala hakuwaepusha na kifo,
bali aliwaangamiza kwa tauni.
51Aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri;
naam, chipukizi wa kwanza kambini mwa Hamu.
52Kisha aliwahamisha watu wake kama kondoo,
akawaongoza jangwani kama kundi la mifugo.
53Aliwaogoza salama, wala hawakuogopa;
lakini bahari iliwafunika maadui zao.
54Aliwaleta katika nchi yake takatifu,
katika mlima aliouteka kwa nguvu yake.
55Aliyafukuza mataifa mbele yao,
akazitoa nchi zao ziwe mali ya Israeli,
akayakalisha makabila ya Israeli mahemani mwao.
56Hata hivyo walimjaribu na kumwasi Mungu Mkuu;
wala hawakuzingatia masharti yake.
57Ila waligeuka na kufanya mabaya kama wazee wao;
wakayumbayumba kama upinde usio imara.
58Walimkasirisha kwa madhabahu zao za miungu;
wakamchochea aone wivu kwa sanamu zao za kuchonga.
59Mungu alipoona hayo, akawaka hasira;
akamkataa Israeli katakata.
60Aliyaacha makao yake kule Shilo,
makao ambamo alikaa kati ya watu.
61Aliiacha ishara ya nguvu yake itekwe,
utukufu wake utiwe mikononi mwa maadui.
62Aliwakasirikia watu wake mwenyewe;
akawatoa waangamizwe kwa upanga.
63Moto ukawateketeza vijana wao wa kiume,
na wasichana wao wakakosa wachumba.
64Makuhani wao walikufa kwa upanga,
wala wajane wao hawakuomboleza.
65Kisha Bwana aliamka kama kutoka usingizini,
kama shujaa aliyechangamshwa na divai.
66Akawatimua maadui zake;
akawatia aibu ya kudumu milele.
67Lakini aliikataa jamaa ya Yosefu,
wala hakulichagua kabila la Efraimu.
68Ila alilichagua kabila la Yuda,
mlima Siyoni anaoupenda.
69Alijenga hapo hekalu lake kubwa kama mbingu,
kama dunia aliyoiweka imara milele.
70Alimchagua Daudi, mtumishi wake,
akamtoa katika kazi ya kuchunga kondoo.
71Alimtoa katika kazi ya kuchunga kondoo na wanakondoo,
awe na jukumu la kuchunga watu wa Yakobo taifa lake.
Achunge Israeli, watu wake Mungu mwenyewe.
72Daudi akawafunza kwa moyo wake wote,
akawaongoza kwa uhodari mkubwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.