Zaburi 140 - Swahili, Common Language Bible

Sala ya kuomba ulinzi wa Mungu(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)

1Ee Mwenyezi-Mungu, uniokoe na watu wabaya,

unikinge na watu wakatili.

2Watu hao huwaza mabaya daima,

huzusha magomvi kila mara.

3 Taz Rom 3:13 Ndimi zao hatari kama za nyoka;

midomoni mwao mna maneno ya sumu kama ya joka.

4Ee Mwenyezi-Mungu, unilinde na makucha ya wabaya;

unikinge na watu wakatili

ambao wamepanga kuniangusha.

5Wenye kiburi wamenitegea mitego,

wametandaza kamba kama wavu,

wameficha mitego njiani wanikamate.

6Namwambia Mwenyezi-Mungu, “Wewe ndiwe Mungu wangu.”

Usikilize, ee Mwenyezi-Mungu, sauti ya ombi langu.

7Ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wangu, mkombozi wangu mkuu,

umenikinga salama wakati wa vita.

8Ee Mwenyezi-Mungu, usiwape waovu wanayotaka;

wala mipango yao mibaya usiifanikishe.

9Hao wanaonizingira wanainua vichwa;

uovu wa maneno yao uwapate wao wenyewe!

10Makaa ya moto yawaangukie;

watumbukizwe mashimoni, wasiinuke tena.

11Wanaowasengenya wengine wasifanikiwe katika nchi;

uovu uwapate wakatili na kuwaangamiza mara!

12Najua Mwenyezi-Mungu hutetea kisa cha wanaoteswa,

na kuwapatia haki maskini.

13Hakika waadilifu watalisifu jina lako;

wanyofu watakaa kwako.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help