1Kisha Bildadi, Mshuhi, akajibu:
2“Utawinda maneno ya kusema hadi lini?
Tafakari vizuri nasi tutasema.
3Kwa nini unatufanya kama ng'ombe?
Mbona unatuona sisi kuwa wapumbavu?
4Wewe unajirarua mwenyewe kwa hasira zako.
Kwani, dunia itaachwa tupu kwa ajili yako
au miamba ihamishwe toka mahali pake?
5 hula viungo vyake.
14Anangolewa katika nyumba aliyoitegemea,
na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15Nyumba yake tupu, wengine wataishi humo;
madini ya kiberiti yametawanywa katika makao yake.
16Yeye ni kama mti uliokauka mizizi,
matawi yake juu yamenyauka.
17Nchini hakuna atakayemkumbuka;
jina lake halitatamkwa tena barabarani.
18Ameondolewa mwangani akatupwa gizani;
amefukuzwa mbali kutoka duniani.
19Hana watoto wala wajukuu;
hakuna aliyesalia katika makao yake.
20Watu wa magharibi wameshangazwa na yaliyompata,
hofu imewakumba watu wa mashariki.
21Hayo ndio yanayowapata wasiomjali Mungu;
hapo ndipo mahali pa wasiomjua Mungu.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.