Zaburi 87 - Swahili, Common Language Bible

Sifa ya Yerusalemu(Zaburi ya Wakorahi. Wimbo)

1Mungu amejenga mji wake

juu ya mlima wake mtakatifu.

2Mwenyezi-Mungu anaupenda mji wa Siyoni,

kuliko makao mengine ya Yakobo.

3Mambo ya fahari yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:

4“Miongoni mwa wale wanijuao mimi,

wapo watu wa Misri na Babuloni.

Kadhalika Filistia, Tiro na Kushi,

wote walizaliwa kwako!”

5Na kuhusu Siyoni itasemwa:

“Siyoni ni mama wa huyu na huyu;

Mungu Mkuu atauthibitisha.”

6Mwenyezi-Mungu ataandika katika kitabu,

atakapoorodhesha watu:

“Huyu amezaliwa huko!”

7Wote wanacheza ngoma na kuimba:

“Siyoni, chanzo chetu ni kwako.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help