Yobu 9 - Swahili, Common Language Bible

Jibu la Yobu

1Kisha Yobu akajibu:

2

9 na wasaidizi wake.

14Nitawezaje basi kumjibu Mungu?

Nitachagua wapi maneno ya kumwambia?

15Ingawa sina hatia, siwezi kumjibu.

Lazima kumwomba anihurumie huyo mshtaki wangu.

16Hata kama ningemwita naye akajibu,

nisingeweza kuamini kuwa ananisikiliza.

17Yeye huniponda kwa dhoruba;

huongeza majeraha yangu bila sababu.

18Haniachi hata nipumue;

maisha yangu huyajaza uchungu.

19Kama ni kushindana, yeye ana nguvu mno!

Na kama ni kutafuta juu ya haki,

nani atakayemleta mahakamani?

20Ingawa sina hatia, maneno yangu yenyewe yangenihukumu;

ingawa sina lawama, angenithibitisha kuwa mpotovu.

21Sina lawama, lakini sijithamini.

Nayachukia maisha yangu.

22Yote ni mamoja, kwa hiyo nasema;

Mungu huwaangamiza wema na waovu.

23Maafa yaletapo kifo cha ghafla,

huchekelea balaa la wasio na hatia.

24Nchi ikitiwa watu waovu katika utawala wa mwovu,

Mungu huyafumba macho ya mahakimu wake!

Kama si yeye afanyaye hivyo, ni nani basi?

25“Siku zangu zaenda mbio kuliko mpiga mbio;

zinakimbia bila kuona faida.

26Zapita kasi kama mashua ya matete;

kama tai anayerukia mawindo yake.

27Nasema: ‘Nitasahau lalamiko langu,

niondoe uso wangu wa huzuni na kuwa na furaha!’

28Lakini nayaogopa maumivu yangu yote,

kwani najua Mungu hataniona kuwa sina hatia.

29Ikiwa nitahukumiwa kuwa na hatia,

ya nini basi nijisumbue bure?

30Hata kama nikitawadha kwa theluji,

na kujitakasa mikono kwa sabuni,

31hata hivyo, atanitumbukiza shimoni kwenye uchafu,

na mavazi yangu yataniona kuwa kinyaa.

32Mungu si mtu kama mimi niweze kumjibu,

hata tuweze kwenda mahakamani pamoja.

33Hakuna msuluhishi kati yetu,

ambaye angeamua kati yetu sisi wawili.

34Mungu na aniondolee hiyo fimbo ya kunipiga,

na kitisho chake kisinitie hofu!

35Hapo ningeweza kusema bila kumwogopa;

kwani sivyo nilivyo nafsini mwangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help