1
23Hiyo ni kazi yake Mwenyezi-Mungu
nayo ni ya ajabu sana kwetu.
24Hii ndiyo siku aliyoifanya Mwenyezi-Mungu;
tushangilie na kufurahi.
25 Taz Mat 21:9; Marko 11:9; Yoh 12:13 Tafadhali utuokoe, ee Mwenyezi-Mungu!
Tafadhali utufanikishe, ee Mwenyezi-Mungu!
26 Taz Mat 21:9; 23:39; Marko 11:9; Luka 13:35; 19:38; Yoh 12:13 Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Mwenyezi-Mungu!
Twawabariki kutoka nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu
27Mwenyezi-Mungu ni Mungu;
yeye ametujalia mwanga wake
Shikeni matawi ya sherehe,
mkiandamana mpaka madhabahuni.
28Wewe ni Mungu wangu, nami ninakushukuru;
ninakutukuza, ee Mungu wangu.
29Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.