Yobu 19 - Swahili, Common Language Bible

Jibu la Yobu

1Kisha Yobu akajibu:

2“Mtaendelea kunitesa mpaka lini,

na kunivunjavunja kwa maneno?

3Mara hizi zote kumi mmenishutumu.

Je, hamwoni aibu kunitendea vibaya?

4Hata kama ingekuwa nimekosa kweli,

kosa langu lanihusu mimi mwenyewe.

5Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;

mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.

6Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,

na kuninasa katika wavu wake.

7Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’

Lakini sijibiwi.

Naita kwa sauti kubwa,

lakini sipati haki yangu.

8Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipite

amezitia giza njia zangu.

9Amenivua fahari yangu;

ameiondoa taji yangu kichwani.

10Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;

tumaini langu amelingoa kama mti.

11Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;

ameniona kuwa kama adui yake.

12Majeshi yake yanijia kwa pamoja;

yametengeneza njia ya kuja kwangu,

yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.

13Mungu amewaweka ndugu zangu mbali nami;

rafiki zangu wakuu wamenitoroka kabisa.

14Jamaa zangu na marafiki hawanisaidii tena.

15Wageni nyumbani mwangu wamenisahau;

watumishi wangu wa kike waniona kuwa mgeni.

Mimi nimekuwa kwao mtu wasiyemjua.

16Namwita mtumishi wangu lakini haitikii,

ninalazimika kumsihi sana kwa maneno.

17Nimekuwa kinyaa kwa mke wangu;

chukizo kwa ndugu zangu mwenyewe.

18Hata watoto wadogo hunidharau,

mara ninapojitokeza wao hunizomea.

19

27Mimi mwenyewe nitakutana naye;

mimi mwenyewe na si mwingine nitamwona kwa macho.

28“Nyinyi mwaweza kujisemea:

‘Tutamfuatia namna gani?

29Tutapataje kwake kisa cha kumshtaki?’

Lakini tahadharini na adhabu.

Chuki yenu yaweza kuwaletea kifo!

Mnapaswa kujua: Mungu peke yake ndiye hakimu.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help