Methali 14 - Swahili, Common Language Bible

1Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,

lakini mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

2Mwenye mwenendo mnyofu humcha Mwenyezi-Mungu,

lakini mpotovu humdharau Mungu.

3Mpumbavu hujiadhibu mwenyewe kwa kuropoka kwake,

lakini mwenye hekima hulindwa na maneno yake.

4Bila ng'ombe wa kulima ghala za mtu ni tupu,

mavuno mengi hupatikana kwa nguvu ya ng'ombe wa kulima.

5Shahidi mwaminifu hasemi uongo,

lakini asiyeaminika hububujika uongo.

6Mwenye dharau hutafuta hekima bure,

lakini mwenye busara hupata maarifa kwa urahisi.

7Ondoka mahali alipo mpumbavu,

maana hapo alipo hamna maneno ya hekima.

8Hekima ya mwenye busara humwonesha njia yake,

lakini upumbavu wa wapumbavu huwadanganya wenyewe.

9Wapumbavu huchekelea dhambi,

bali wanyofu hupata fadhili kwa Mungu.

10Moyo waujua uchungu wake wenyewe,

wala mgeni hawezi kushiriki furaha yake.

11Nyumba ya mtu mwovu itabomolewa,

lakini hema ya wanyofu itaimarishwa.

12

33Hekima imo moyoni mwa mtu mwenye busara;

haipatikani kamwe mioyoni mwa wapumbavu.

34Uadilifu hukuza taifa,

lakini dhambi ni balaa kwa taifa lolote.

35Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima,

lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help