Zaburi 125 - Swahili, Common Language Bible

Usalama wa watu wa Mungu(Wimbo wa Kwenda Juu)

1Wanaomtegemea Mwenyezi-Mungu, wako kama mlima Siyoni,

ambao hautikisiki bali wabaki imara daima.

2Kama Yerusalemu inavyozungukwa na milima,

ndivyo Mwenyezi-Mungu awazungukavyo watu wake,

tangu sasa na hata milele.

3Waovu hawataendelea kutawala nchi ya waadilifu;

wasije waadilifu nao wakafanya maovu.

4Ee Mwenyezi-Mungu, uwe mwema kwa watu wema,

kwa wale wanaozitii amri zako.

5Lakini wanaogeuka na kufuata njia zao mbaya

uwakumbe pamoja na watenda maovu.

Amani iwe na Israeli!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help