Ezekieli 17 - Swahili, Common Language Bible

Mfano wa tai na mzabibu

1Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2“Wewe mtu! Tega kitendawili, uwaambie fumbo Waisraeli.

3Waambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:

Kulikuwa na tai mmoja mkubwa sana

aliyekuwa na mabawa makubwa,

yenye manyoya marefu mengi

yenye rangi za kila aina.

Tai huyo aliruka mpaka mlimani Lebanoni,

akatua juu ya kilele cha mwerezi;

4akakwanyua tawi lake la juu zaidi,

akalipeleka katika nchi ya wafanyabiashara,

akaliweka katika mji wao mmoja.

5Kisha akachukua mmea mchanga nchini Israeli,

akaupanda katika ardhi yenye rutuba

ambako kulikuwa na maji mengi.

6Mmea ukakua ukawa mzabibu

wa aina ya mti utambaao;

matawi yake yakamwelekea,

na mizizi yake ikatanda chini yake.

Mzabibu ukachipua matawi na majani mengi.

7Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa;

alikuwa na mabawa makubwa ya manyoya mengi.

Basi, ule mzabibu ukamtandia mizizi yake,

ukamwelekezea matawi yake,

ili aumwagilie maji.

8Mzabibu ulikuwa umetolewa kitaluni mwake

ukapandikizwa penye udongo mzuri na maji mengi,

ili upate kutoa matawi na kuzaa matunda

uweze kuwa mzabibu mzuri sana!

9Sasa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nakuuliza:

Je, mzabibu huo utaweza kustawi?

Je, hawatangoa mizizi yake

na kuozesha matunda yake

na matawi yake machanga kuyanyausha?

Hakutahitajika mtu mwenye nguvu au jeshi

kuungoa kutoka humo ardhini.

10Umepandikizwa, lakini, je, utastawi?

Upepo wa mashariki uvumapo juu yake utanyauka;

utanyauka papo hapo kwenye kuta ulikoota.”

Maelezo yake

11Kisha neno la Mwenyezi-Mungu likanijia:

12

24Ndipo miti yote nchini itajua kuwa mimi Mwenyezi-Mungu huiporomosha miti mirefu na kuikuza miti mifupi. Mimi hukausha miti mibichi na kustawisha miti mikavu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema hayo na nitayafanya.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help