Isaya 9 - Swahili, Common Language Bible

Mtoto amezaliwa kwetu

1

17Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu hawahurumii vijana wao,

hana huruma juu ya yatima na wajane wao;

kwani hakuna hata mmoja amchaye Mungu,

kila mtu husema uongo.

Hata hivyo, hasira yake haijatulia,

bado ameunyosha mkono wake.

18Uovu huwaka kama moto

uteketezao mbigili na miiba;

huwaka kama moto msituni,

na kutoa moshi mzito upandao angani juu.

19Kwa ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi

nchi imechomwa moto,

na watu ni kama kuni za kuuwasha.

Hakuna mtu anayemhurumia ndugu yake;

20wananyanganya upande mmoja na hawatosheki;

wanakula upande mwingine lakini hawashibi.

Kila mmoja anamshambulia mwenzake.

21Manase dhidi ya Efraimu,

Efraimu dhidi ya Manase

na wote wawili dhidi ya Yuda.

Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia,

bado ameunyosha mkono wake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help