1
17Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu hawahurumii vijana wao,
hana huruma juu ya yatima na wajane wao;
kwani hakuna hata mmoja amchaye Mungu,
kila mtu husema uongo.
Hata hivyo, hasira yake haijatulia,
bado ameunyosha mkono wake.
18Uovu huwaka kama moto
uteketezao mbigili na miiba;
huwaka kama moto msituni,
na kutoa moshi mzito upandao angani juu.
19Kwa ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi
nchi imechomwa moto,
na watu ni kama kuni za kuuwasha.
Hakuna mtu anayemhurumia ndugu yake;
20wananyanganya upande mmoja na hawatosheki;
wanakula upande mwingine lakini hawashibi.
Kila mmoja anamshambulia mwenzake.
21Manase dhidi ya Efraimu,
Efraimu dhidi ya Manase
na wote wawili dhidi ya Yuda.
Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia,
bado ameunyosha mkono wake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.