Zaburi 99 - Swahili, Common Language Bible

Mungu mtawala mkuu

1Mwenyezi-Mungu anatawala,

mataifa yanatetemeka!

Ameketi juu ya viumbe vyenye mabawa,

nayo dunia inatikisika!

2Mwenyezi-Mungu ni mkuu katika Siyoni;

ametukuka juu ya mataifa yote.

3Wote na walisifu jina lake kuu la kutisha.

Mtakatifu ndiye yeye!

4Ee mfalme mkuu, mpenda uadilifu!

Umethibitisha haki katika Israeli;

umeleta uadilifu na haki.

5Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;

angukeni kifudifudi mbele zake.

Mtakatifu ndiye yeye!

6Mose na Aroni walikuwa makuhani wake;

Samueli alikuwa miongoni mwa waliomlilia.

Walimlilia Mwenyezi-Mungu naye akawasikiliza.

7Alisema nao katika mnara wa wingu;

waliyazingatia matakwa yake na amri alizowapa.

8Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza;

kwao ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliwaadhibu kwa makosa yao.

9Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;

abuduni katika mlima wake mtakatifu!

Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ni mtakatifu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help