Zaburi 36 - Swahili, Common Language Bible

Uovu wa binadamu(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi, mtumishi wa Mwenyezi-Mungu)

1 Taz Rom 3:18 Dhambi huongea na mtu mwovu,

ndani kabisa moyoni mwake;

jambo la kumcha Mungu halimo kabisa kwake.

2Mwovu hujipendelea mwenyewe,

hufikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.

3Kila asemacho ni uovu na uongo;

ameacha kutumia hekima na kutenda mema.

4Alalapo huwaza kutenda maovu,

hujiweka katika njia isiyo njema,

wala haachani na uovu.

Wema wa Mungu

5Fadhili zako ee Mwenyezi-Mungu zaenea hata mbinguni;

uaminifu wako wafika mawinguni.

6Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,

hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.

Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama

7Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!

Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.

8Wawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako;

wawanywesha kutoka mto wa wema wako.

9Wewe ndiwe asili ya uhai;

kwa mwanga wako twaona mwanga.

10Uendelee kuwafadhili wale wanaokutambua;

uzidi kuwa mwema kwa wanyofu wa moyo.

11Usikubali wenye majivuno wanivamie,

wala watu waovu wanikimbize.

12Kumbe watendao maovu wameanguka;

wameangushwa chini, hawawezi kuinuka.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help